Posts

Mtihani wa Kiswahili Kidato cha Nne 2024 NECTA Majibu

Image
Sehemu A (Alama 16) 1. Katika kipengele I hadi X chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu kwenye kijitabu chako cha kujibia. (i) Vifuatavyo ni vyanzo vya misimu, isipokuwa: A Tanakali sauti au milio A B Sayansi na Teknolojia C Shughuli maalumu D Utani katika jamii E Mabadiliko ya historia (ii) Neno lenye mofu ya mtendwa ni lipi kati ya haya? A Aliyetembea B Alimkimbilia B C Alivyotembea D Atakayetembea E Ametembea (iii) Msaada wako umenifaa sana. Asante! Neno "Asante!" ni aina gani ya neno? A Nomino B Kivumishi C Kielezi D Kitenzi E Kihisishi E (iv) Tamathali ipi ya semi hukipa kitu kisicho binadamu sifa ya ubinadamu? A Taniaba B Tashihisi B C Tashibiha D Takriri E Tabaini (v) "Wanafunzi wa Kidato cha Pili wamepigiwa ngoma." Kauli hii inaonesha hali gani? A Kutendana B Kutendeka C Kutendewa C D Kutendwa E Kutendea (v) "Wanafunzi wa Kidato cha Pili wamepigwa ngoma." Kauli hii inaonesha hali gani? A Kutendana B Kutendeka C Kutendewa D Kuten...

Mambo ya Kuzingatia Katika Uandishi wa Dayolojia

Image
Fafanua mambo tisa ya muhimu ya kuzingatia katika uandishi wa dayolojia . (NECTA Kidato cha Nne 2024) Dayolojia ni mazungumzo ya kupokezana kati ya watu wawili au zaidi. Mazungumzo hayo yanaweza kuwa ya ana kwa ana au kwa njia ya simu. Pia huweza kuandikwa au kuzungumzwa. Dayolojia zinazoandikwa ni pamoja na: michezo ya redio, tamthilia na maigizo. Mambo tisa muhimu ya kuzingatia katika uandishi wa dayolojia ni: 1.  Jambo linalomsukuma mwandishi Mwandishi lazima awe na jambo linalomsukuma katika uandika dayolojia yake. Jambo hilo linaweza kuwa: kutoa elimu kuhusu jambo fulani, umasikini, na jambo lolote alilonalo. 2.  Mahitaji ya jamii anayoiandikia Mwandishi lazima atambue mahitaji ya jamii yake. Kama jamii yake inaelekea katika uchaguzi mkuu, basi inatakiwa atakachokiandika kihusiane na uchaguzi kwani ndiyo hitaji kuu la wakati huo. Mahitaji yanaweza yakawa mengi kwa wakati mmoja. 3.  Kutoa maelezo ya ufafanuzi katika mabano Maelezo ya ufafanuzi katika mabano yana leng...