Uhakiki wa Riwaya ya Mirathi ya Hatari
Mwandishi: C. G. Mung’ong’o Mwaka: 1977 Mhakiki: Mwalimu Makoba Utangulizi Mirathi ya hatari kisomwe kwa tahadhari. Yale yanayojadiliwa humo, ni mambo ya kufikirika ambayo katika dunia hii iliyojaa uhalisia hayana nafasi. Kitabu hiki kisiposomwa kwa tahadhari, kinaweza kusababisha changamoto tatu: Kwanza, wanafunzi wataamini habari za uchawi kuwa ni za kweli. Wataanza kuiona dunia kama sehemu ya miujiza na si uhalisia wa bidii ya kufanya mambo. Pili, wanafunzi watapatwa na hofu, watakapougua, watahisi pengine wamechezewa ilhali kuugua ni hali ya kawaida katika maisha na vipo visababishi mbalimbali wakiwamo mbu waenezao malaria. Changamoto ya tatu bado haijajulikana na inaninyima usingizi! Kwa hivyo unaposoma kitabu hiki, na unapohakiki riwaya hii, tambua jambo moja, yanayosemwa humu hayawezi kutokea katika ulimwengu wa kawaida. Dunia yetu inaongozwa na kanuni nayo sayansi imethibitisha uchawi haupo. Jamii za kiafrika bado zinaamini katika ushirikina, mwandishi, anaonyesha imani hiyo,...