Posts

Matokeo NECTA Kidato cha Sita 2026

Image
NECTA Wametangaza matokeo ya kidato cha sita, wapo wanafunzi waliofanya vyema, lakini wapo wanafunzi ambao wameshindwa kufikia malengo yao. Tazama Hapa Matokeo NECTA Kidato cha Sita 2026 Wanafunzi waliofanya vizuri tunawapongeza na kuwatakia kila la heri katika safari yao ya masomo yanayoendelea. Wanafunzi waliofanya vibaya, wasikate tamaa, bado wana nafasi yakurudia mitihani yao. Tafsiri ya kufanya vibaya ni kushindwa kufikia malengo. Kwa mfano, mwanafunzi aliyekuwa na malengo ya kwenda chuo kikuu, pale anapopata chini ya D mbili, hujiona kama ambaye hajafikia malengo kwani anatakiwa aongeze D nyingine moja. Huu si muda wa kukata tamaa, bali ni muda wa kurudia tena. Mwanafunzi aliyepata C moja na E, huyo anahesabiwa kuwa na sifa za kwenda chuo kikuu hata kama hajapata D mbili. Katika kurudia mitihani, wanatakiwa watambue kwamba, mtaala sasa umebadilika, vitabu ni vipya siyo vile ambavyo walisoma zamani. Hata hivyo, masomo haya yanaeleweka vyema na yeyote anayetemaani kufaulu vyema ana...

Maswali ya Usaili TAKUKURU Oral Interview

Image
Baada ya usaili wa kuandika , wanaofaulu huingia hatua ya pili ambayo ni usaili wa mahojiano. Katika usaili huu, swali bado ni lilelile, maswali gani huulizwa? Makala hii inaeleza maswali yanayoulizwa katika usaili wa TAKUKURU . Lugha inayotumika hapa ni lugha ya kiingereza. Katika saili zao, huweza kutumia lugha yoyote kati ya Kiingereza au Kiswahili. Kuna wakati wanaweza kuongea kiingereza halafu wakabadilika na kutumia Kiswahili. Katika maswali haya, swali la kwanza ni lazima utakutana nalo, hivyo fanya mazoezi ya kutosha. 1. Tell me about yourself Thank you, Chairperson and honorable members of the panel, for this opportunity to introduce myself. My name is Daud Makoba Mhuli. I hold a degree from the University of Dar es Salaam, For years, I have worked as a teacher and content creator. Through this work, I have sharpened two critical skills that are vital for a TAKUKURU officer: deep analytical investigation and the ability to educate communities. I am here today because my person...

Uhakiki wa riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo

Image
Wasiliana na Mwalimu ili Kujiunga Darasa la Uhakiki wa Vitabu vyote vya Fasihi Mtaala Mpya kwa Kugusa Hapa Mwandishi: Euphrase Kezilahabi Mwaka: 1975 Mhakiki: Mwalimu Makoba Nilipofika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya masomo yangu, mtu wa kwanza kutamani kumuona alikuwa ni Profesa Euphrase Kezilahabi. Nilimsoma katika kazi zake mbalimbali ikiwamo hii ya Dunia Uwanja wa Fujo. Nilianza msako mara moja wa kumtafuta Profesa Kezilahabi bila mafanikio. Baadaye niligundua kupitia kwa mwalimu wangu M.M. Mulokozi, ambaye aliwahi kuwa mwanafunzi wa Kezilahabi kwamba, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kilimfuta kazi Kezilahabi miaka mingi iliyopita! Mwishoni mwa miaka ya 1990 Kezilahabi aliomba likizo ya miaka miwili kwenda kufundisha Botswana . Alikubaliwa na akaenda Botwana mwaka 1995. miaka miwili ilipokwisha Botswana walimwongezea muda, akakiomba Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimwongezee muda lakini akakataliwa na kuambiwa arejee mara moja. Aliposhindwa kurejea alifutwa kazi na kujikuta ha...