Uhakiki wa Riwaya ya Joka la Mdimu
Mwandishi: Abdallah Saffari Mhakiki: Mwalimu Makoba Simulizi kwa ufupi Joka la mdimu ni aina ya nyoka ambaye hukaa katika majani ya kijani. Kwa kuwa nyoka huyu hufanana na majani, ni ngumu sana kumtambua. Joka hili la mdimu linafananishwa na viongozi. Viongozi hawa wanafanana na sisi kwa kila kitu hivyo ni vigumu mno kutambua hatari yao ya uongozi mbaya, rushwa, mauaji na ulaghai. Cheche anaumia akishiriki maonyesho ya sherehe za uhuru. Kwa sababu ya kukosekana kwa fedha za kigeni, inashindikana kumpeleka Uingereza kutibiwa, na japo serikali inawajibika kumtibia, haionekani kufanya hivyo wala kujali. Baba yake anavamia benki, anapata fedha na kufanikiwa kumpelekea Uingereza kutibiwa. Maudhui Dhamira Hali ngumu ya maisha Katika riwaya hii tunauona ugumu wa maisha. Mhusika Jinja Maloni anafanya kazi yoyote ilimradi mkono uende kinywani. Anafanya kazi ya kuchimba makaburi na kupakua vyoo. Hali hii ngumu ya maisha inasababishwa na uongozi mbaya, viongozi wameshindwa kuzuia rushwa, mfumuk...