Posts

Mtihani wa Kiswahili NECTA Kidato cha Nne 2025 Maswali na Majibu

Image
SEHEMU A (Alama 16) Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Katika vipengele (i) hadi (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu cha chaguo cha kujibia. (i) Ni taarifa zipi zinaweza kupatikana katika kamusi kati ya hizi? A. Neno, maana, matamshi na matumizi ya semi B. Maana, neno, mazungumzo na matumizi ya semi C. Matumizi ya semi, matamshi, maana na mazungumzo D. Matamshi, mazungumzo, maana na kidahizo E. Kidahizo, matamshi, mazungumzo na semi Jibu: D (ii) “Juma anaendesha baiskeli yake polepole.” Kiarifu cha sentensi hii kimejengwa na mfuatano upi wa vipashio? A. Kiima, chagizo na shamirisho B. Kitenzi kishirikishi, shamirisho na chagizo C. Kiarifu, kiima na chagizo D. Shamirisho, chagizo na kitenzi kikuu E. Kitenzi kikuu, shamirisho na chagizo Jibu: E (iii) “Tutakuja kumpokea kwenye uwanja wa ndege.”   Kazi ya kielezi kinachojitokeza kwenye sentensi hii ni ipi kati ya hizi? A. Kueleza idadi B. Kueleza mahali C. Kueleza namna D. Kueleza w...

Sarufi ya Kiswahili | Kiswahili Kidato cha Tano Mada ya 1

Image
Sarufi ni kanuni zinazoongoza matumizi ya lugha. Dhana za fonimu na alofoni za lugha ya Kiswahili Dhana za fonimu na alofoni hujitokeza katika tawi la sarufi matamshi. Vilevile, tawi hilo huitwa fonolojia. Fonolojia ni tawi la sarufi linalohusika na uchunguzi na uchanganuzi wa mfumo wa sauti za lugha mahususi. Mfumo wa sauti za lugha hujengwa na vipashio mbalimbali. Kipashio cha msingi katika fonolojia hujulikana kama fonimu. Fonimu ni sauti zote za lugha zenye uwezo wa kupambanua au kutofautisha maana katika maneno ya lugha fulani mahususi. Fonimu za lugha zimegawanyika katika makundi mbalimbali ambayo ni: - Konsonanti - Irabu - Viyeyusho Fonimu hutofautiana kwa idadi kutoka lugha moja hadi nyingine. Mathalani, Kiswahili kina jumla ya fonimu thelathini zilizogawanyika katika makundi yaliyotajwa. Katika Kiswahili, kuna irabu tano ambazo ni: /i/, /ɛ/, /u/, /ɔ/, /a/; Konsonanti ishirini na tano ambazo ambazo ni /p, b, t, d, k, g, f, v, θ, s, z, ʃ, ʒ, tʃ, dʒ, h, m, n, ɲ, ŋ, l, r, j, w/; n...