Mtihani wa Kiswahili NECTA Kidato cha Nne 2025 Maswali na Majibu
SEHEMU A (Alama 16) Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Katika vipengele (i) hadi (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu cha chaguo cha kujibia. (i) Ni taarifa zipi zinaweza kupatikana katika kamusi kati ya hizi? A. Neno, maana, matamshi na matumizi ya semi B. Maana, neno, mazungumzo na matumizi ya semi C. Matumizi ya semi, matamshi, maana na mazungumzo D. Matamshi, mazungumzo, maana na kidahizo E. Kidahizo, matamshi, mazungumzo na semi Jibu: D (ii) “Juma anaendesha baiskeli yake polepole.” Kiarifu cha sentensi hii kimejengwa na mfuatano upi wa vipashio? A. Kiima, chagizo na shamirisho B. Kitenzi kishirikishi, shamirisho na chagizo C. Kiarifu, kiima na chagizo D. Shamirisho, chagizo na kitenzi kikuu E. Kitenzi kikuu, shamirisho na chagizo Jibu: E (iii) “Tutakuja kumpokea kwenye uwanja wa ndege.” Kazi ya kielezi kinachojitokeza kwenye sentensi hii ni ipi kati ya hizi? A. Kueleza idadi B. Kueleza mahali C. Kueleza namna D. Kueleza w...