Jinsi ya kuandaa Somo na Kuwasilisha Oral Interview Ajira za Walimu
Nililia kwa uchungu, sikuamini kwamba, yote niliyomfanyia Ashura, mchepuko niliyekuwa na malengo naye, aliyaona hayafai. Ni mimi ndiye niliyempa mbinu zote za kufaulu usaili ajira za walimu , bidii yote na uwekezaji niliofanya, Ashura kaniacha! Niliisoma upya meseji yake ya mwisho, “Mwalimu Makoba, asante kwa msaada wako, ni wewe uliyenisaidia mpaka nimepata ajira ya ualimu mkoani Dodoma, hata hivyo, siwezi tena kuendelea na wewe kwa sababu mbili: kwanza, una mke na mimi sipo tayari kuwa mchepuko, ninahitaji maisha yangu; pili, nimepata mume mkulima wa zabibu tena anayeijua dini vizuri, wewe hueleweki dini yako; japo umesoma, lakini elimu imeshindwa kukubadilisha, bado unafuata tamaduni za Kisukuma ikiwemo kuabudu mizimu!” Nilipomaliza kuisoma, nililia upya, mke akaamka na kuniuliza shida nini? Nilidanganya, “Nimemkumbuka marehemu bibi!” Nilikumbuka jambo moja muhimu, msafara wa Rais ungepita karibu na mtaa wetu, na rais angesimama kusikiliza kero za wanachi. Nilitembea haraka nam...